Muigizaji Kingwendu ni miongoni mwa mastaa ambao wamechukua headline za kugombea Ubunge kwenye Uchaguzi Mkuu 2015 kama Afande Sele, Professor Jay, Muigizaji Frank na wengine.
Mchekeshaji na muigizaji Kingwendu anagombea ubunge kwenye jimbo la Kisarawe mkoa wa Pwani kupitia tiketi ya CUF, Kingwendu
hakuwahi kusikika kabisa tangu kampeni zianze, lakini kabla October 20
2015 Jumapili haijafika leo amekaa na sisi kwenye exclusive na millardayo.com na kutupa mipango yake kwenye Siasa inavyokwenda.
‘Tangu
kampeni zianze huku hali ni nzuri na nina faida kubwa ya kushinda sasa
hivi Wazaramo wameamka wanataka mabadiliko, muda mrefu wamewapa umaskini
wamewadharirisha na wamewanyima elimu lakini mimi huku nimewafufua
vizuri wamenielewa na mikakati yangu… watu wamenielewa vizuri na wako
tayari kupiga kura kwa Kingwendu’- Kingwendu.
“Nitakapoingia
Bungeni sitofanya kazi ya uchekeshaji, kazi iliyonileta bungeni ni
kutetea wananchi, kuwaletea maendeleo na kufuta kero zote za wananchi…
si vyema tena kuingia kwenye majukwaa na kukata viuno kwa kuwa tayari
nitakuwa Mheshimiwa“
Kwenye sentensi nyingine Kingwendu ameyaongea haya >>> “Nitakapokuwa
Bungeni nitaepukana na ile sauti niliyokuwa naitumia katika sanaa
nitakuwa na sauti ya kawaida, nitajenga hoja za Msingi ninataka kutoa
mfano kwa viongozi waliopita Kisarawe habari ndio hiyo“- Kingwendu.
0 comments:
Post a Comment