Thursday, 22 October 2015

Entertainment Meek Mill. Vs. Wale kwenye mitandao ya kijamii, warushiana maneno… kisa?!

Leave a Comment
Jana rapper kutoka kwenye kundi la Maybach Music Group (MMG) Wale aliitembelea studio ya Power 105.1 kwa ajili ya interview na kipindi cha The Breakfast Club… kwenye interview hiyo Wale aliongelea vitu vingi ikiwemo kuzindua nyimbo nne mpya kupitia kipindi hicho na badaaye kugusia issue iliyotokea kati ya Meek Mill na Drake.
Alipoulizwa kuhusu mtazamo wake kuhusiana na beef ya Meek Mill na Drake, Wale alionekana kumsuport sana Drake na sio msani mwenzake kutoka MMG, Meek Mill… akiwa kwenye interview hiyo Wale alisema…
waale3
>>>Nadhani Meek alikuja na penseli kwenye pambano la bunduki, hata hajaja na kisu, kaja na penseli na karatasi kabisa, akajaribu kumkata na karatasi, huwezi kushindana na mtu kama Drake…” <<< Wale.
Wale aliendelea kumwagia sifa Drake kwa kudai kuwa, Drake aliaachia nyimbo mbili za kumponda Meek Mill kwa kutumia njia yenye manufaa zaidi, kuweka diss track zake kwenye mtandao wa Apple Music ambapo watu iliwabidi wanunue kusikia alisema nini kuhusu Meek Mill, wakati Meek Mill aliiachia diss track yake kupitia kipindi cha redio.
waale4
Kwa upande wa Meek Mill, hili jambo halijamfuraisha kabisa, na ukiitembelea Instagram page yake sasa hivi utakutana na post ndefu sana ya kumjibu Wale huku akidai Wale ameamua kumuongelea ili ajiweke headlines na wimbo wake mpya isitoshe pia ni mtu mwenye wivu…
WALE
WALE2
Wale hakukaa kimya, akachukuwa time na post #tweets kadhaa kupitia ukurasa wake wa Twitter...
If You Enjoyed This, Take 5 Seconds To Share It

0 comments: